MADHUMUNI YA KUANZISHA UWAWASE GROUP
1 Madhumuni
ya umoja huu ni kuhakikisha kuwa
wazalishaji wa Sembe/Dona na wamiliki wa mashine za kuzalishaSembe tunakuwa na
chombo cha kutusemea kwa umoja wetu na kutufanya tuwe pamoja na kutuwezesha
kusaidiana pale inapo tokea kunahaja ya kusaidiana, kwa ugonjwa au kifo. Pia ni
kuhakikisha tunaendesha umoja wetu huu kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, mbali na yote umoja wetu utalazimika kufanya
mambo yafuatayo;-
a. Kununua
mahindi popote yatakapo patikana ndani na nje ya nchi.
b. Kuuza
sembe na dona ndani na nje ya inchi kwa kufuata sheria za nchi.
c. Kutii
mamlaka za serikali na kufuata maagizo yake.pamoja na kupokea maelekezo toka
manispaa kwa utekelezaji.
d. Kutetea
na kulinda maslai ya wana uwawase
e. Kukusanya
ada na michango mingine itakayoidhinishwa na mkutano mkuu kwa wana umoja wote. Ili kuboresha utendaji
wa umoja wetu.
f. Kutekeleza
maamuzi ya takayo pitishwa kwenye mkutano mkuu wa wanaumoja .






0 comments:
Post a Comment