Monday, May 2, 2016

MALENGO YA UMOJA WA UWAWASE GROUP

MALENGO YA UMOJA WA UWAWASE GROUP

11.    Kuwaunganisha wamiliki na mashine na wazalishaji Sembe/Dona katika mkoa wa Dar es Salaam na vuinga vyake.

2.    Kuhakikisha tunazalisha Sembe bora ili kulinda afya za walaji.

3.    Kutafuta na kufuatilia soko la malighafi (mahindi) popote ndani na nje ya Tanzania ili kukidhi haja na mahitaji ya wanaUwawase Group.

4.    Kutafuta na Kufuatilia Soko la Sembe/Dona popote ndani na nje ya Tanzania kwa ajili ya wanaUwawase Group kuuza Sembe/Dona zao.

5.    Kuwa na soko la bei moja wakati wa kununua mahindi na kuuza Sembe/Dona.

6.    Kutetea na kulinda maslahi ya wanachama.

7.    Kukusanya kiingilio, Ada na mapato mengine yatakayowaletea maendeleo ya wanaumoja.

8.    Kubuni, kuzianzisha na kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza mapato ya Chama na kuboresha maisha ya wanachama.

9.    Kuitangaza na kuiunganisha Uwawase na taasisi za serikali na zisizo za serikali ili kupata huduma stahiki kwa Chama na wanachama.

10.                       Kufanya Uwawase kuwa katika kundi la wawekezaji wa ndani wa viwanda vidogo vya kati katika uzalishaji wa usambazaji wa Sembe/dona bora ndani na nje ya Tanzania.

11.                       Kutafuta njia rahisi ya kupata mitaji ya kustawisha viwanda na biashara ya wanauwawase group.

12.                       Kuwa taasisi/Umoja mkubwa unaojitosheleza katika tasinia hii ya uwezeshaji wa viwanda vya kuongeza dhamani ya mahindi.
Share:

0 comments:

Post a Comment