UENDESHAJI WA MASUALA YA KIFEDHA NDANI YA UWAWASE GROUP
VYANZO VYA MAPATO.
1. Kiingilio.
2. Ada.
3. Mikopo
ya bank/Taasisi za fedha.
4. Msaada
toka kwa wafadhili
5. Mauzo
ya nakala ya katiba.
6. Mauzo
ya vitabu vya sheria ndogondogo za umoja.
7. Michango
mbalimbali kutoka kwa taasisi zisizokuwa za serikali za ndani na nje ya nchi,
vitu halisi au fedha.
4.1
MATUMIZI YA MAPATO.
Umoja
huu uta hakikisha una yatumia ipasavyo mapato yote yaliyopatikana kwa njia tajwa
hapo juu yaani (4.0 1hadi 7)kwa kufanya mambo yafuatayo:-
1. Kulipa
pango la ofisi ya Uwawase Group.
2. Kumpa
rambirambi mfiwa au marehemu kwataratibu tuliojiwekea.
3. Kusaidia
jitihada za kutafuta malighafi (mahindi) popote pale ili kuwafanya wanaumoja
kupata mahindi hasa kipindi cha upungufu wa mahindi.
4. Ikibidi
hata kufanya mawasiliano na nje ya nchi kufanikisha kupata mahindi.
5. Kuendesha
shughuli zote za ofisi ya UWAWASE GROUP, pamoja na kugharamia matumizi ya
ofisi.
6. Kulipa
watumishi wa ofisi kama Karani/Secretary, mlinzi, na viongozi kwa shughuli
maalum za ofisi na ufuatiliaji nje ya ofisi kwa manuafaa ya umoja wetu.
7. Ikifikia
wakati tuibue vitega uchumi mbalimbali kuimarisha mfuko wetu.
8. Kugharamia
mikutano yote ya Uwawase Group.
9. Kutimiza
malengo ya umoja yaliyopitishwa na mkutano mkuu.
4.2
VITU HALISIYA.
a) Iwapo
mtu au taasisi itafanya shughuli na UWAWASE GROUP na ikafanikiwa kujitolea
vifaa au pesa, kwaajili ya utekelezaji wa mpango wowote UWAWASE GROUP haitalipa
wala kugharamia uharibifu wowote utakaojitokeza.
b) UWAWASE
GROUP itabaki kuwa ndio mmiliki mkuu wa mali na wanaumoja wake,bila kuingiliana
na taasisi yoyote ile iliyoshirikishwa.
4.3
ASASI ZA FEDHA.
a) Iwapo
mkutano mkuu ukiona kuna umuhimu wa kupatapesa kutoka benki kwa haraka katika
umoja wetu kwaajili ya kufanya jambo kwa maramoja na lenye malengo mema
kimaendeleo, basi mkutano mkuu utatoa idhini kwa kamati ya utendaji kufanya
hivyo chini ya taratibu ambazo mkutano mkuu utakuwa umeziweka/kuridhia kwa
pamoja.
b) Wanaumoja
watakaopitisha azimio hili la kukopa pesa au bank katika Taasisi kipesa
zilizoruhusiwa kisheria lazima liwe theluthi tatu ya wanaumoja wote.
4.4
UHIFADHI WA FEDHA.
1. Umoja
utahifadhi pesa zake bank.
2. Sehemu
ya pesa ndogondogo zinazohitajika kwa matumizi ya kiofisi yatahifadhiwa kwa
taratibu zitakazowekwa na uongozi kwa mtunza fedha,
3. Tunaweza
kuwekeza fedha kwa kununuwa hisa au mali isiyo hamishika kama nyumba, kiwanja/shamba
kwa makubaliano ya wanaumoja kupitia mkutano mkuu.
4. Mwaka
wa fedha wa umoja utaanza Januari na kuishia DIsemba.
5. Umoja
utaandaa hesabu zake na kuzitunza kwa utaratibu ulioandaliwa na wanaumoja
wenyewe.
6. Kamati
ya mipango, uchumi nafedha ya umoja itapitia taarifa ya fedha kila baada ya
miezi mitatu na kuiwasilisha kwenye mkutano wa wanaumoja.
7. Wajumbe
wa kamati yamipango, uchumi na fedha watakuwa na idhini ya kupitia manunuzi,
matumizi, na mapato yote yaliyofanyika kwenye umoja.
8. Ukaguzi,kuundwe
kamati ya dharura ya ukaguzi wa hesabu za mwaka kutoka kwa wana umoja wenyewekamati
hiyo isizidi watu watano kwa ukaguzi wa hesabu za ndani(mtaalam wa
hesabu/mahesabu).
9. Muda
wa kamati ya ukaguzi utakoma baada ya kumaliza hesabu hizo ndani ya mwezi
mmoja.
10. Gharama
za kamati ya ukaguzi zitalipwa na mfuko wa umoja wenyewe.









0 comments:
Post a Comment