UONGOZI NA KAMATI ZA UONGOZI WA UWAWASE GROUP
USIMAMIZI/UWONGOZI.
1. Madaraka
makuu yanayo husu UWAWASE GROUP yatakuwa kwa wana umoja wenyewe kwenye mikutano
mikuu.
2. Kutakuwa
na mikutano mikuu ya UWAWASE GROUP (3)
i)
Mkutano mkuu ya mwaka.
ii) Mkutano
kila baada ya miezi mitatu.
iii) Mkutano
wa dharura.
3.2
Kufanya uchaguzi wa viongozi wa UWAWASE
GROUP.
3.3
Kujadili na kutoa mapendekezo ya miradi
ya UWAWASE GROUP.
3.4
Kuidhinisha mauzo au manunuzi ya mali za
UWAWASE GROUP.
3.5
Kutaundwa kamati ndogondogo za uwongozina
zitakuwa na mamlaka ya kutambuliwa na wana UWAWASE GROUP.
VIONGOZI.
UWAWASE
GROUP, Itaongozwa na viongozi wafuatao:-
1. Mwenyekiti
2. Makamu
mwenyekiti
3. Katibu
4. Katibu
msaidizi
5. Mtunza
Hazina
Viongozi
hawa watapigiwa kura ya siri na wajumbe wa mkutano mkuu wa umoja .
6.1
Muda wa uongozi wa UWAWASE GROUP ni miaka mitatu tu.
6.2
Idadi ya wapiga kura kwenye mkutano mkuu italazimika wajumbe wafike zaidi ya nusu
ya
wanaumoja wote.
1.3 Wajumbe
wa mkutano mkuu watateua kamati itakayosimamia mambo ya katiba, sheria
nanidhamu ya umoja.
6.4
Kamati ya utendaji itakuwa na wajibu wa kuunda kamati mbalimbali zitakazo
imarisha
utendaji
wa umoja.
6.5
Kiongozi anaweza kuongoza mihula miwili kama ataonekena anafaa kufanya hivyo na
wanaumoja.
WAJIBU
WA VIONGOZI.
MWENYEKITI.
a. Mwenyekiti;
ataendesha vikao vyote vya umoja ndie msemaji mkuu katika mikutano yote na
kutoa miongozo kwa kila jambo ndani na nje ya mkutano wa umoja.
b. Mwenyekiti;
msaidizi huyu atafanya shughuli zote za mwenyekiti kwa kutumwa na mwenyekiti au
pindi mwenyekiti anapokuwa hayupo.
KATIBU.
a. Katibu,
atakuwa ndiemtendaji mkuu wa umoja kwa shughuli zote zakiutendajikwa wana umoja
pia ataandika taarifa zote za mikutano na kutunza kumbukumbu zote za vikao
halali vya umoja,na atakuwa na mawasiliano ya marakwamara kati ya uongozi na wanaumoja kuhusu taarifa zozote zinazo wahusu
wanaumoja.
b. Katibu
msaidizi atafanya shughuli zote za katibukwa kushirikiana na pindi katibu mkuu
atakapokuwa hayup atakaimu.
MTUNZA
HAZINA.
a. Atahakikisha
anafuata taratibu zote za uhifadhiwa fedha za umoja.
b. Atapokea
pesa na kutoa risiti kwa mwanaumoja yeyote atakae toa pesa zihusuzo umoja.
c. Atafanya
malipo pale atakapo takiwa kufanya hivyo na kamati ya fedha ya umoja kwa
kushirikiana na watia saini baada ya kulipishwa na kamati ya utendaji.
d. Atahakikisha
hesabu zote za fedha ya umoja ndiye atazitolea maelezo ya mapato na matumizi
pale atakapotakiwa kufanya hivyo na kikao halali cha umoja.
e. Atatunza
vitabu vyote vya risiti na hesabu za umoja.
f. Atakusanya
na kupeleka pesa bank kila mara.
g. Ataandaa
hesabu zote za umoja na kuziwakilisha kwenye kikao/mkutano husika.
h. Atashauri
kamati ya fedha juu ya matumizi ya umoja yenye tija.
i.
Atashirikiana na kamati ya fedha kuandaa
bajeti ya matumizi ya umoja pale inapotakiwa kufanya hivyo.
KAMATI
YA UTENDAJI.
Kamati
hii ndiyo kamati ambayo inatakiwa kuwa makini kwa kuhakikisha inafanya mambo ya
kiutendajizaidi.
1. Itapokea
na kutekeleza maelekezo yote kutoka mkutano mkuu wa umoja
2. Itafuatilia
kazi na maelekezo mbalimbali yanayo husu umoja wetu
3. Itahusika
kutoa maelekezo ya kiutendaji kwa kamati mbalimbali za umoja wetu.
4. Itaitisha
mkutano wa dharura kujadili jambo lolote jipya kwa wanaumoja.
5. Itakuwa
na jukumu la kumuhidhinisha mwanaumoja mpya baada ya kupokea barua yake ya
maombi ya kujiunga na umoja iliyokuwisha jadiliwa na kamati ya katiba na sheria.
6. Itabuni
na kuanzisha mradi au jambo lolote maslahi kwa wanaumoja baada ya kukubaliwa na
mkutano mkuu.
7. Itazingatia
maslai ya umoja zaidi kuliko vinginevyo.
KAMATI
YA KATIBA SHERIA NA NIDHAMU.
Kamati
hii itakuwa ndiyo msingi wa umoja wetu kwa kuhakikisha inafanya mambo yake kwa
werevu mkubwa huku ikijuwa kuwa ndio
tegemeo kubwa la kisheria la umoja, nayo itateuliwa kupitia mkutano mkuu wa
wanaumoja, hatahivyo itakuwa kamati huru, kamati hii itasimamia uchaguzi wa
viongozi kipindi cha uchaguzi, pia
itafanya yafuatayo:-
a. Kusimamia
utekelezwaji wa maelekezo ya katiba ya umoja.
b. Kusimamia
maboresho ya katiba ya umoja pindi itakapo lazimika kufanya hivyo.
c. Kuhakikisha
kila kiongozi/mwanaumoja anatii na kufuata sheria hizo
d. Kudhibiti
mwiingiliano wa uongozi katika umoja.
e. Kuunda
sheria ndogondogo zitakazo ongoza umoja wetu.
f. Kuhakikisha
viongozi wa umoja wanatii na kuilinda katiba katika utendaji wao
g. Kusimamia
adhabu kwa mwana umoja kutokana na kosa alilofanya.
h. Kushauriana
na kamati ya utendaji juu ya kufanya mikataba mbalimbali inayohusu umoja wetu.
i.
Kupokea na kujadili barua ya barua ya
maombi mapya kabla ya kuidhinishwa na kamati ya utendaji.
j.
Kamati hii pamoja na kuwa huru itafanya
kazi kwa karibu na chini ya kamati ya utendaji kwa maslahi ya wanauwawase
group.






0 comments:
Post a Comment